Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 73

Zaburi 73:1-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.

Read Zaburi 73Zaburi 73
Compare Zaburi 73:1-18Zaburi 73:1-18