Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 72

Zaburi 72:3-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
4Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
5Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
6Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
7Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.

Read Zaburi 72Zaburi 72
Compare Zaburi 72:3-10Zaburi 72:3-10