Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 71

Zaburi 71:5-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Maana wewe ni tumaini langu, Bwana Yahwe. Nimekuamini wewe siku zote tangu nilipokuwa mtoto.
6Nimekuwa nikisaidiwa na wewe tangu tumboni; wewe ndiye yule uliyenitoa tumboni mwa mama yangu; sifa zangu zitakuhusu wewe siku zote.
7Mimi ni mfano bora kwa watu wangu; wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.
8Mama yangu atajawa na sifa zako, siku zote akikuheshimu.
9Usinitupe katika siku za miaka ya uzee wangu; usiniache wakati nguvu zangu zitakapoisha.
10Maana adui zangu wanazungumza kuhusu mimi; wale wanao fatilia uhai wangu wanapanga njama pamoja.
11Wao husema, “Mungu amemuacha; mfuateni na mumchukue, maana hakuna yeyote awezaye kumuokoa yeye.”
12Mungu, usiwe mbali nami; Mungu wangu, harakisha kunisaidia mimi.
13Waaibishwe na kuharibiwa, wale walio adui wa uhai wangu; wavishwe laumu na kudharauliwa, wale watafutao kuniumiza.
14Lakini nitakutumainia wewe siku zote na nitakusifu wewe zaidi na zaidi.
15Kinywa changu kitaongea kuhusu haki yako na wokovu wako mchana kutwa, ingawa ziwezi kuzielewa maana ni nyingi mno.
16Nitakuja na matendo yenye nguvu ya Bwana Yahwe; nitataja haki yako, yako pekee.
17Mungu, tangu ujana wangu wewe umenifundisha; hata sasa ninatangaza matendo yako ya ajabu.
18Hakika, hata niwapo mzee na mvi kichwani, Mungu, usiniache mimi, kama ambavyo nimekuwa nikitanga nguvu yako kwa vizazi vijavyo, na uweza wako kwa yeyote ajaye.

Read Zaburi 71Zaburi 71
Compare Zaburi 71:5-18Zaburi 71:5-18