Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 71

Zaburi 71:1-13

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Katika wewe, Yahwe, napatakimbilio salama; usiniache niaibishwe.
2Uniokoe na kunifanya salama katika haki yako; geuzia sikio lako kwangu.
3Uwe kwagu mwamba kwa ajili ya kimbilio salama ambako naweza kwenda siku zote; wewe umeamuru kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
4Uniokoe mimi, Mungu wangu, kutoka katika mkono wa asiye haki na katili.
5Maana wewe ni tumaini langu, Bwana Yahwe. Nimekuamini wewe siku zote tangu nilipokuwa mtoto.
6Nimekuwa nikisaidiwa na wewe tangu tumboni; wewe ndiye yule uliyenitoa tumboni mwa mama yangu; sifa zangu zitakuhusu wewe siku zote.
7Mimi ni mfano bora kwa watu wangu; wewe ni kimbilio langu lenye nguvu.
8Mama yangu atajawa na sifa zako, siku zote akikuheshimu.
9Usinitupe katika siku za miaka ya uzee wangu; usiniache wakati nguvu zangu zitakapoisha.
10Maana adui zangu wanazungumza kuhusu mimi; wale wanao fatilia uhai wangu wanapanga njama pamoja.
11Wao husema, “Mungu amemuacha; mfuateni na mumchukue, maana hakuna yeyote awezaye kumuokoa yeye.”
12Mungu, usiwe mbali nami; Mungu wangu, harakisha kunisaidia mimi.
13Waaibishwe na kuharibiwa, wale walio adui wa uhai wangu; wavishwe laumu na kudharauliwa, wale watafutao kuniumiza.

Read Zaburi 71Zaburi 71
Compare Zaburi 71:1-13Zaburi 71:1-13