Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 6

Zaburi 6:2-7

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Unihurumie, Yahwe, kwa maana ni dhaifu; uniponye, Yahweh, kwa kuwa mifupa yangu ina tikisika.
3Moyo wangu pia umesumbuka sana. Lakini wewe, Yahweh, mpaka lini hali hii itaendelea?
4Rudi, Yahweh! uniokoe. Uniokoe kwa sababu ya uaminifu wa agano lako!
5kwa kuwa kifoni hakuna kumbukumbu lako. Kuzimuni ni nani atakaye kushukuru?
6Nimechoshwa na kuugua kwangu. Ninalowanisha kitanda changu kwa machozi usiku kucha; ninaosha kiti changu kwa machozi.
7Macho yangu yanafifia kwa kulia sana; yanazidi kuwa dhaifu kwa sababu ya adaui zangu.

Read Zaburi 6Zaburi 6
Compare Zaburi 6:2-7Zaburi 6:2-7