Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 69

Zaburi 69:23-35

Help us?
Click on verse(s) to share them!
23Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.

Read Zaburi 69Zaburi 69
Compare Zaburi 69:23-35Zaburi 69:23-35