Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 69

Zaburi 69:18-27

Help us?
Click on verse(s) to share them!
18Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.

Read Zaburi 69Zaburi 69
Compare Zaburi 69:18-27Zaburi 69:18-27