Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 69

Zaburi 69:15-19

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.

Read Zaburi 69Zaburi 69
Compare Zaburi 69:15-19Zaburi 69:15-19