Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 68

Zaburi 68:5-13

Help us?
Click on verse(s) to share them!
5Baba wa yatima, na mwamuzi wa wajane, ni Mungu anayeishi mahali patakatifu.
6Mungu huwaweka wakiwa katika familia; yeye huwafungua wafungwa kwa kuimba bali waasi huishi katika ardhi kavu.
7Mungu, wewe ulipoenda mbele ya watu wako, ulipotembea kupitia jangwani, Selah
8nchi ilitetemeka; mbingu pia zilidondosha mvua katika uwepo wa Mungu, uweponi mwa Mungu wakati alipokuja Sinai, uweponi mwa Mungu, Mungu wa Israeli.
9Wewe, Mungu, ulituma mvua nyingi; uliuimarisha urithi wako wakati ulipokuwa umechoka.
10Watu wako waliishi humo; Wewe, Mungu, uliutoa kwa wema wako kwa maskini.
11Bwana alitoa amri, na wale walio zitangaza walikuwa ni jeshi kuu.
12Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia, na wanawake wakisubiri nyumbani kuvigawana wao na familia zao vilivyotekwa nyara.
13Njiwa walio vikwa fedha wakiwa na mabawa ya njano ya dhahabu. Wakati baadhi ya watu wakikaa kati ya mifugo ya kondoo, kwa nini umefanya haya?

Read Zaburi 68Zaburi 68
Compare Zaburi 68:5-13Zaburi 68:5-13