Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 66

Zaburi 66:4-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4Nchi yote watakuabudu wewe na watakuimbia wewe; wataliimbia jina lako.” Selah
5Njoni na mtazame kazi za Mungu; yeye anatisha katika matendo yake awatendeayo wanadamu.
6Aligeuza bahari kuwa nchi kavu; wao walitembea kwa mguu juu ya mto; huko tulishangilia katika yeye.
7Yeye anatawala milele kwa nguvu zake; macho yake yanachunguza mataifa; waasi wasijivune. Selah
8Mtukuzeni Mungu, enyi watu wa mataifa yote, sauti ya sifa zake isikike.
9Yeye atuwekaye hai, naye hairuhusu miguu yetu iteleze.
10Kwa maana wewe, Mungu, umetupima sisi, wewe umetupima kama inavyopimwa fedha.
11Wewe ulituingiza sisi kwenye wavu; uliweka mzigo mzito viunoni mwetu.
12Wewe uliwafanya watu wasafiri juu ya vichwa vyetu; tulipita motoni na majini, lakini ukatuleta mahali pa wazi palipo salama.
13Nitaingia nyumbani mwako nikiwa na sadaka ya kuteketezwa; nitakulipa viapo vyangu
14ambavyo midomo yangu iliahidi na kinywa changu kiliongea nilipokuwa katika dhiki.
15Nitakutolea sadaka ya kuteketezwa ya wanyama wanene pamoja na harufu nzuri ya kondoo waume; Nitatoa ng'ombe na mbuzi. Selah
16Njoni, msikie, ninyi nyote mnao mwabudu Mungu, nami nitatangaza yale yeye aliyoitendea roho yangu.
17Nilimlilia kwa kinywa changu, naye alipendezwa na ulimi wangu.
18Kama ningelikuwa na dhambi ndani ya moyo wangu, Bwana asingenisikiliza.

Read Zaburi 66Zaburi 66
Compare Zaburi 66:4-18Zaburi 66:4-18