Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 62

Zaburi 62:7-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
8Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. Selah
9Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
10Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
11Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
12Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.

Read Zaburi 62Zaburi 62
Compare Zaburi 62:7-12Zaburi 62:7-12