Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 61

Zaburi 61:1-7

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Sikia kulia kwangu, shughulikia maombi yangu.
2Kutokea mwisho wa nchi nitakuita wewe wakati moyo wangu umeelemewa; uniongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi.
3Maana wewe umekuwa kimbilio langu la usalama, nguzo imara dhidi ya adui.
4Uniache niishi hemani mwako milele! Nipate kimbilio salama chini ya makazi ya mbawa zako. Selah
5Kwa kuwa wewe, Mungu, umesikia viapo vyangu, wewe umenipa mimi urithi wa wale wanao liheshimu jina lako.
6Wewe utaongeza maisha ya mfalme; miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.
7Yeye atabakia mbele ya Mungu milele.

Read Zaburi 61Zaburi 61
Compare Zaburi 61:1-7Zaburi 61:1-7