Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 5

Zaburi 5:2-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
3Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
4Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
5Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
6Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
7Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
8Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
9Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
10Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.

Read Zaburi 5Zaburi 5
Compare Zaburi 5:2-10Zaburi 5:2-10