Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 59

Zaburi 59:11-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
11Usiwaue, hivyo watu watasahau. Uwatawanye kwa nguvu zako na uwaangushe, Bwana ngao yetu.
12Kwa ajili ya dhambi za midomo yao na maneno ya midomo yao, wakamatwe katika majivuno yao, na kwa laana na uongo ambao wao huelezea.
13Uwamalize katika gadhabu yako, uwamalize ili kwamba wasiwepo tena; wajue kuwa Mungu anatawala katika Yakobo na mwisho wa nchi. Selah
14Wakati wa jioni wao hurudi, wakibweka kama mbwa wakiuzungukia mji.
15Wanatangatanga wakitafuta chakula na wanabweka kama mbwa kama hawajatosheka.
16Lakini nitaimba kuhusu nguvu zako, na asubuhi nitaimba kuhusu upendo wako imara! maana umekuwa mnara wangu mrefu na kimbilio la usalama katika siku ya taabu.

Read Zaburi 59Zaburi 59
Compare Zaburi 59:11-16Zaburi 59:11-16