5Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
6Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! Selah
7Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
8Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
9Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
10Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
11Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.