Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 57

Zaburi 57:4-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
5Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
6Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! Selah
7Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
8Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
9Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
10Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
11Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.

Read Zaburi 57Zaburi 57
Compare Zaburi 57:4-11Zaburi 57:4-11