Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 50

Zaburi 50:4-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.

Read Zaburi 50Zaburi 50
Compare Zaburi 50:4-18Zaburi 50:4-18