2Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.