Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 44

Zaburi 44:9-25

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14Umetufaya kituko kati ya mataifa,...
15Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.

Read Zaburi 44Zaburi 44
Compare Zaburi 44:9-25Zaburi 44:9-25