Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 44

Zaburi 44:2-17

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. Selah
9Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14Umetufaya kituko kati ya mataifa,...
15Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.

Read Zaburi 44Zaburi 44
Compare Zaburi 44:2-17Zaburi 44:2-17