Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 38

Zaburi 38:7-19

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
8Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
9Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
10Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
11Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
12Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
13Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
14Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
15Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
16Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
17Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
18Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
19Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.

Read Zaburi 38Zaburi 38
Compare Zaburi 38:7-19Zaburi 38:7-19