7Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
8Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
9Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
10Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
11Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.