Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 37

Zaburi 37:6-14

Help us?
Click on verse(s) to share them!
6Yeye ataidhihilisha haki yako kama mchana na usafi wako kama mwangaza wa mchana.
7Uwe kumya mbele za Yahwe na umsubiri yeye kwa uvumilivu. Usikasirike ikiwa kuna mtu anafanikiwa kwa kile afanyacho, au afanyapo njama za uovu.
8Usikasilile na kugadhabika. Usiogope. Hii huleta matatizo tu.
9Watendao maovu watafutiliwa mbali, bali wale wamngojao Yahwe watairithi nchi.
10Katika muda mfupi mtu mwovu atatoweka; wewe utatazama mahali pake, wala hautamuona.
11Lakini wapole watairithi nchi nao watafurahia katika mafanikio makubwa.
12Mtu mwovu hupanga njama kinyume na mwenye haki na kumsagia meno.
13Bwana humcheka, kwa maana anaona siku yake inakuja.
14Waovu wametoa nje panga zao na wametayarisha pinde zao ili kuwaangamiza wanyonge na wahitaji, na kuwaua wenye haki.

Read Zaburi 37Zaburi 37
Compare Zaburi 37:6-14Zaburi 37:6-14