Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 37

Zaburi 37:3-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Uwamini Mungu na kufanya yaliyo mema; uishi katika nchi na uongezeke katika imani.
4Kisha ufurahi mwenyewe katika Yahwe, naye atakupa matamanio ya moyo wako.
5Umkabidhi njia zako Yahwe; uamini katika yeye, naye atatenda kwa niaba yako.
6Yeye ataidhihilisha haki yako kama mchana na usafi wako kama mwangaza wa mchana.
7Uwe kumya mbele za Yahwe na umsubiri yeye kwa uvumilivu. Usikasirike ikiwa kuna mtu anafanikiwa kwa kile afanyacho, au afanyapo njama za uovu.
8Usikasilile na kugadhabika. Usiogope. Hii huleta matatizo tu.
9Watendao maovu watafutiliwa mbali, bali wale wamngojao Yahwe watairithi nchi.
10Katika muda mfupi mtu mwovu atatoweka; wewe utatazama mahali pake, wala hautamuona.
11Lakini wapole watairithi nchi nao watafurahia katika mafanikio makubwa.
12Mtu mwovu hupanga njama kinyume na mwenye haki na kumsagia meno.
13Bwana humcheka, kwa maana anaona siku yake inakuja.
14Waovu wametoa nje panga zao na wametayarisha pinde zao ili kuwaangamiza wanyonge na wahitaji, na kuwaua wenye haki.
15Panga zao zitawaua wenyewe, na pinde zao zitavunjika.
16Ni bora kuwa mwenye haki maskini kuliko tajiri mwenye mali nyingi.
17Kwa maana mikono ya watu waovu itavunjika, bali Yahwe huwasaidia watu wenye haki.
18Yahwe huwalinda watu wasio na lawama siku hadi siku, na urithi wao utakuwa wa milele.

Read Zaburi 37Zaburi 37
Compare Zaburi 37:3-18Zaburi 37:3-18