Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 37

Zaburi 37:16-30

Help us?
Click on verse(s) to share them!
16Ni bora kuwa mwenye haki maskini kuliko tajiri mwenye mali nyingi.
17Kwa maana mikono ya watu waovu itavunjika, bali Yahwe huwasaidia watu wenye haki.
18Yahwe huwalinda watu wasio na lawama siku hadi siku, na urithi wao utakuwa wa milele.
19Hawata aibika siku mbaya zijapo. Wakati wa njaa ufikapo wao watakuwa na chakula cha kutosha.
20Bali waovu wataangamia. Maadui wa Yahwe watakuwa kama vile utukufu wa malisho; watamalizwa na kupotezwa katika moshi.
21Mtu mwovu hukopa lakini halipi, bali mtu mwenye haki ni mkarimu na hutoa.
22Wale walio barikiwa na Mungu watairithi nchi; wale aliowalaani watafutiliwa mbali.
23Hatua za mwanadamu zinaimarishwa na Yahwe, mtu ambaye njia zake zinakubalika machoni pa Mungu.
24Ajapojikwaa, hataanguka chini, kwa kuwa Yahwe anamshikilia kwa mkono wake.
25Nilikuwa kijana na sasa ni mzee; sijawahi kumuona mtu mwenye haki ametelekezwa wala watoto wake kuombaomba mkate.
26Wakati wote yeye ni mkarimu na hukopesha, nao watoto wake hufanyika baraka.
27Acha uovu na ufanye yaliyo mema; ndipo utakapokuwa salama milele.
28Kwa maana Yahwe hupenda haki naye hawaachi wafuasi waaminifu. Wao hutunzwa milele, lakini uzao wa waovu utafutiliwa mabli.
29Wenye haki watairithi nchi na kuaa huko milele.
30Mdomo wa mwenye haki huongea hekima na huongeza haki.

Read Zaburi 37Zaburi 37
Compare Zaburi 37:16-30Zaburi 37:16-30