Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 37

Zaburi 37:14-18

Help us?
Click on verse(s) to share them!
14Waovu wametoa nje panga zao na wametayarisha pinde zao ili kuwaangamiza wanyonge na wahitaji, na kuwaua wenye haki.
15Panga zao zitawaua wenyewe, na pinde zao zitavunjika.
16Ni bora kuwa mwenye haki maskini kuliko tajiri mwenye mali nyingi.
17Kwa maana mikono ya watu waovu itavunjika, bali Yahwe huwasaidia watu wenye haki.
18Yahwe huwalinda watu wasio na lawama siku hadi siku, na urithi wao utakuwa wa milele.

Read Zaburi 37Zaburi 37
Compare Zaburi 37:14-18Zaburi 37:14-18