Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 35

Zaburi 35:18-23

Help us?
Click on verse(s) to share them!
18Nami nitakushukuru wewe katika kusanyiko kubwa; nitakusifu kati ya watu wengi.
19Usiwaache maadui zangu wadanganyifu kufurahi juu yangu; usiwaache waendelee na mipango yao ya uovu.
20Kwa maana hawaongei amani, bali wanabuni maneno ya uongo kwa wale wanaoishi kwa amani katika ardhi yetu.
21Midomo yao inapaza sauti ikinishtaki; wakisema, Aha, Aha, macho yetu yameona.”
22Yahwe wewe umeona, usikae kimya; Bwana, usiwe mbali nami.
23Inuka mwenyewe na usimame kunitetea; Mungu wangu na Bwana wangu, unitetee.

Read Zaburi 35Zaburi 35
Compare Zaburi 35:18-23Zaburi 35:18-23