Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 34

Zaburi 34:3-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.

Read Zaburi 34Zaburi 34
Compare Zaburi 34:3-15Zaburi 34:3-15