Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 33

Zaburi 33:1-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Furahini katika Yahwe, ninyi wenye haki; kusifu kwa wenye haki kwa faa sana.
2Mshukuruni Bwana kwa kinubi; mwimbieni sifa kwa kinubi chenye nyuzi kumi.
3Mwimbieni yeye wimbo mpaya; pigeni kwa ustadi na muimbe kwa furaha.
4Kwa kuwa maneno ya Mungu ni ya hakika, na kila afanyacho ni haki.
5Yeye hupenda haki na kutenda kwa haki. Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe.
6Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa, na nyota zote ziliumbwa kwa pumzi ya mdomo wake.
7Yeye huyakusanya maji ya baharini kama rundo; naye huiweka bahari katika ghala.
8Basi ulimwengu wote umwogope Yahwe; wenyeji wote wa ulimwengu wamuhofu yeye.
9Kwa maana yeye alisema, na ikafanyika; aliamuru, na ikasimama mahali pake.
10Yahwe huvunja muungano wa mataifa; naye huishinda mipango ya wanadamu.
11Mipango ya Yahwe husimama milele, mipango ya moyo wake ni kwa ajili ya vizazi vyote.
12Limebarikiwa taifa ambalo Mungu wao ni Yahwe, watu ambao yeye amewachagua kama warithi wake.

Read Zaburi 33Zaburi 33
Compare Zaburi 33:1-12Zaburi 33:1-12