Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 30

Zaburi 30:3-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Yahwe, wewe umeitoa roho yangu kuzimuni; nawe umeniweka hai mbali na kaburi.
4Mwimbieni sifa Yahwe, ninyi waaminifu wake! Mshukuruni Bwana mkumbukapo utakatifu wake.
5Kwa kuwa hasira yake ni ya muda tu; bali neema yake yadumu milele. Kilio huja usiku, bali furaha huja asubuhi.
6Kwa ujasiri nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7Yahwe, kwa neema yako uliniweka mimi kama mlima imara; lakini ulipouficha uso wako, nilisumbuka.
8Nilikulilia wewe, Yahwe, na kuomba msaada kwa Bwana wangu!
9Kuna faida gani katika kifo changu, kama nitaenda kaburini? Je, mavumbi yatakusifu wewe? Yatatangaza uaminifu wako?
10Sikia, Yahwe, na unihurumie! Yahwe, uwe msaidizi wangu.
11Wewe umegeuza kuomboleza kwangu kuwa kucheza; wewe umeyaondoa mavazi yangu ya magunia na kunivisha furaha.
12Hivyo sasa utukufu wangu utakuimbia sifa wewe na hautanyamaza; Yahwe Mungu wangu, nitakushukuru wewe milele!

Read Zaburi 30Zaburi 30
Compare Zaburi 30:3-12Zaburi 30:3-12