Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 30

Zaburi 30:1-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Nitakutukuza wewe, Yahwe, kwa kuwa umeniinua na haujawaruhusu maadui zangu juu yangu.
2Yahwe Mungu wangu, nilikulilia wewe kwa ajili ya msaada, nawe ukaniponya.
3Yahwe, wewe umeitoa roho yangu kuzimuni; nawe umeniweka hai mbali na kaburi.
4Mwimbieni sifa Yahwe, ninyi waaminifu wake! Mshukuruni Bwana mkumbukapo utakatifu wake.
5Kwa kuwa hasira yake ni ya muda tu; bali neema yake yadumu milele. Kilio huja usiku, bali furaha huja asubuhi.
6Kwa ujasiri nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7Yahwe, kwa neema yako uliniweka mimi kama mlima imara; lakini ulipouficha uso wako, nilisumbuka.
8Nilikulilia wewe, Yahwe, na kuomba msaada kwa Bwana wangu!
9Kuna faida gani katika kifo changu, kama nitaenda kaburini? Je, mavumbi yatakusifu wewe? Yatatangaza uaminifu wako?
10Sikia, Yahwe, na unihurumie! Yahwe, uwe msaidizi wangu.
11Wewe umegeuza kuomboleza kwangu kuwa kucheza; wewe umeyaondoa mavazi yangu ya magunia na kunivisha furaha.

Read Zaburi 30Zaburi 30
Compare Zaburi 30:1-11Zaburi 30:1-11