Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 22

Zaburi 22:10-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Nimekwisha tupwa kwako wewe tokea tumboni; wewe ni Mungu wangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu!
11Usiwe mbali na mimi, kwa kuwa shida ikaribu; hayupo hata mmoja wa kusaidia.
12Maksai wengi wananizunguka mimi; maksai wenye nguvu ya Bashan wananizunguka mimi.
13Wao wanafungua midomo yao kwangu kama simba aungurumaye akirarua windo lake.
14Ninamwagwa nje kama maji, na mifupa yangu yote imeteguka. Moyo wangu ni kama nta; nao unayeyuka ndani ya sehemu zangu za ndani.
15Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.

Read Zaburi 22Zaburi 22
Compare Zaburi 22:10-20Zaburi 22:10-20