Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 18

Zaburi 18:9-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
9Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
11Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
12Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
14Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
15Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
16Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.

Read Zaburi 18Zaburi 18
Compare Zaburi 18:9-16Zaburi 18:9-16