Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 18

Zaburi 18:33-43

Help us?
Click on verse(s) to share them!
33Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
34Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
35Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
36Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
37Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
38Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
39Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
40Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
41Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
42Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
43Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.

Read Zaburi 18Zaburi 18
Compare Zaburi 18:33-43Zaburi 18:33-43