10Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
11Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
12Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
13Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!