Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 147

Zaburi 147:10-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Hapati furaha katika nguvu ya farasi, wala haridhii miguu imara ya mwanadamu.
11Yahwe huridhia katika wale wanao muheshimu yeye, watumainio katika uaminifu wa agano lake.
12Msifuni Yahwe, Yerusalemu, msifuni Mungu wenu, Sayuni.
13Maana yeye huyakaza mapingo ya malango yako, huwabariki watoto wako kati yako.
14Huletamafanikio ndani ya mipaka yako, hukutosheleza kwa ngano bora.
15Huipeleka amri yake juu ya nchi, amri zake hupiga mbio sana.
16Huifanya theluji kama sufu, huitawanya barafu kama majivu.

Read Zaburi 147Zaburi 147
Compare Zaburi 147:10-16Zaburi 147:10-16