Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 145

Zaburi 145:10-21

Help us?
Click on verse(s) to share them!
10Vyote ulivyo viumba vitakushukuru wewe, Yahwe; waaminifu wako watakutukuza wewe.
11Waaminifu wako watanena juu ya utukufu wa ufalme wako, na watahubiri juu ya nguvu zako.
12Watayafanya matendo makuu ya Mungu ya julikane na wanadamu na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
13Ufalme wako ni wa milele, na mamlaka yako ya dumu kizazi hata kizazi.
14Yahwe huwategemeza wote waangukao na huwainua wote walioinama chini.
15Macho ya wote yanakungoja wewe; nawe huwapa chakula chao kwa wakati sahihi.
16Huufungua mkono wako na hukidhi haja ya kila kiumbe hai.
17Yahwe ni mwenye haki katika njia zake zote na neema katika yote afanyayo.
18Yahwe yu karibu na wote wamwitao, wale wamwitao yeye katika uaminifu.
19Hutimiza haja za wale wanao mheshimu yeye; husikia kilio chao na kuwaokoa.
20Yahwe huwalinda wale wampendao, lakini atawaangamiza waovu wote.
21Kinywa changu kitazinena sifa za Yahwe; wanadamu wote na walitukuze jina lake takatifu milele na milele.

Read Zaburi 145Zaburi 145
Compare Zaburi 145:10-21Zaburi 145:10-21