5Nakumbuka siku za zamani zilizopita; nayatafakari matendo yako yote; nawaza juu ya utimilifu wako.
6Nakunyoshea mikono yangu katika maombi; nafsi yangu inakuonea kiu katika nchi kavu. Selah
7Unijibu upesi, Yahwe, kwa sababu roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, vinginevyo nitakuwa kama wale waendao chini shimoni.
8Unifanye kusikia uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi, maana ninakuamini wewe. Unionyeshe njia niipasayo kutembea kwayo, kwa maana nakuinulia wewe nafsi yangu.
9Uniokoe dhidi ya adui zangu, Yahwe; nakimbilia kwako ili nijifiche.