Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 140

Zaburi 140:3-12

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Ndimi zao zinajeruhi kama nyoka; sumu ya fira imo midomoni mwao. Selah
4Ee Yahwe, unilinde dhidi ya mikono ya waovu; unikinge na vurugu za watu wanaopanga kuniangusha.
5Wenye majivuno wameweka mtego kwa ajili yangu; wameeneza nyavu; wameweka kitanzi kwa ajili yangu. Selah
6Nilimwambia Yahwe, “Wewe ni Mungu wangu; usikie kilio changu unihurumie.”
7Ee Yahwe, Bwana wangu, wewe ni mwenye nguvu uwezaye kuniokoa; hunifunika ngao kichwa changu siku ya vita.
8Ee Yahwe, usiyatimize matakwa ya waovu; usiruhusu njama zao kufanikiwa. Selah
9Wale wanao nizunguka huinua vichwa vyao; madhara ya midomo yao wenyewe na yawafunike.
10Makaa ya moto na yawaangukie; uwatupe motoni, kwenye shimo refu, wasiweze kuinuka tena.
11Watu wenye ndimi na wasifanywe salama juu ya nchi; na uovu umuwinde kumpiga mtu mwenye vurugu mpaka afe.
12Ninajua kuwa Yahwe atahukumu kwa haki walioteswa, na kuwa atawapa haki wahitaji.

Read Zaburi 140Zaburi 140
Compare Zaburi 140:3-12Zaburi 140:3-12