19Ee Mungu, kama ungewaua waovu; ondokeni kwangu enyi watu wenye vurugu.
20Wanakuasi wewe na kutenda udanganyifu; adui zako wananena uongo.
21Je, siwachukii hao, wale wakuchukiao Yahwe? Je, siwadharau wale wanao inuka dhidi yako?
22Nawachukia kabisa; wamekuwa adui zangu.
23Ee Mungu, unichunguze na kuujua moyo wangu; unijaribu na uyajue mawazo yangu.
24Uone kama kuna njia ya uovu ndani yangu, na uniongoze katika njia ya milele.