4Makabila huenda juu Yerusalemu, makabila ya Yahwe; kama ushuhuda wa Israeli, kulishukuru jina la Yahwe.
5Huko viliwekwa viti vya hukumu, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
6Ombeni kwa ajili ya amani ya Yerusalemu! “Wote wakupendao wawe na amani.
7Amani iwepo ndani ya kuta zako ili ikutetee, na wawe na amani ndani ya ngome zako.”
8Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema, “Amani iwe ndani yenu.”