Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:98-115

Help us?
Click on verse(s) to share them!
98Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.
99Ninauelewa zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa maana ninazitafakari amri za agano lako.
100Ninaelewa kuliko wale wanaonizidi umri; hii ni kwa sababu nimeyashika maagizo yako.
101Nimeiepusha miguu yangu na kila njia ya uovu ili niweze kulitii neno lako.
102Sijaenda kinyume na amri zako za haki, kwa maana wewe umenifundisha.
103Ni jinsi gani maneno yako ni matamu kwenye majaribu yangu, naam, matamu kuliko asali kinywani mwangu!
104Kupitia maagizo yako ninapata utambuzi; kwa hiyo kila njia isiyo ya kweli.
105Neno lako ni taa ya mguu miguu yangu na mwanga wa njia yangu.
106Nimeapa na nimethibitisha, kuwa nitazitii amri za haki yako.
107Nimeteswa sana; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika neno lako.
108Yahwe, tafadhali pokea dhabihu yangu ya hiari ya kinywa changu, na unifundishe amri zako za haki.
109Uhai wangu ziku zote uko mkononi mwangu, lakini bado sisahau sheria yako.
110Waovu wamenitegea mtego, lakini sijapotea mbali na maagizo yako.
111Nimezifanya amri za agano lako kama urithi wangu milele, maana hizo ni furaha ya moyo wangu.
112Moyo wangu umewekwa kuzitii sheria zako milele mpaka mwisho kabisa. SAMEKH.
113Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
114Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
115Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:98-115Zaburi 119:98-115