Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:51-71

Help us?
Click on verse(s) to share them!
51Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
52Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
53Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.
54Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu katika nyumba ninayoishi kwa muda.
55Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
56Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
57Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
58Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
59Nilizichunguza njia zangu na kugeuzia miguu yangu kwenye amri za agano lako.
60Naharakisha na sichelewi kuzishika amri zako.
61Kamba za waovu zimenifunga; nami sijaisahau sheria yako.
62Katikati ya usiku ninaamka kukushukuru wewe kwa sababu ya amri za haki yako.
63Ninaurafiki na wale wanao kuabudu wewe, wale wote watiio maagizo yako.
64Yahwe, nchi, imejaa uaminifu wa agano lako; unifundishe sheria zako. TETH.
65Wewe umemtendea mema mtumishi wako, Yahwe, sawasawa na neno lako.
66Unifundishe utambuzi sahihi na uelewa, kwa kuwa nimeamini katika amri zako.
67Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
68Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.
69Wenye kiburi wamenichafua kwa uongo, lakini niliyashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.
70Mioyo yao ni migumu, lakini ninafurahia katika sheria yako.
71Ni vizuri kwangu kuwa nimeteseka ili niweze kujifunza sheria zako.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:51-71Zaburi 119:51-71