Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:44-118

Help us?
Click on verse(s) to share them!
44Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.
45Nitaenenda salama, maana ninayatafuta maagizo yako.
46Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
47Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.
48Nitaziinulia mikono yangu amri zako, nizipendazo; nitazitafakari sheria zako. ZAYIN.
49Kumbuka ahadi yako kwa mtumishi wako kwa sababu umenipa tumaini.
50Hii ni faraja yangu katika mateso: kuwa ahadi yako imeniweka hai.
51Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
52Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
53Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.
54Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu katika nyumba ninayoishi kwa muda.
55Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
56Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
57Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
58Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
59Nilizichunguza njia zangu na kugeuzia miguu yangu kwenye amri za agano lako.
60Naharakisha na sichelewi kuzishika amri zako.
61Kamba za waovu zimenifunga; nami sijaisahau sheria yako.
62Katikati ya usiku ninaamka kukushukuru wewe kwa sababu ya amri za haki yako.
63Ninaurafiki na wale wanao kuabudu wewe, wale wote watiio maagizo yako.
64Yahwe, nchi, imejaa uaminifu wa agano lako; unifundishe sheria zako. TETH.
65Wewe umemtendea mema mtumishi wako, Yahwe, sawasawa na neno lako.
66Unifundishe utambuzi sahihi na uelewa, kwa kuwa nimeamini katika amri zako.
67Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
68Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.
69Wenye kiburi wamenichafua kwa uongo, lakini niliyashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.
70Mioyo yao ni migumu, lakini ninafurahia katika sheria yako.
71Ni vizuri kwangu kuwa nimeteseka ili niweze kujifunza sheria zako.
72Maagizo yatokayo kinywani mwako ni ya thamani zaidi kwangu kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha. YOD.
73Mikono yako imeniumba na kunitengeneza; unipe uelewa ili niweze kujifunza amri zako.
74Wale wanao kucha wewe watafurahi wanionapo kwa sababu ninapata tumaini katika neno lako.
75Ninajua, Yahwe, kuwa amri zako ni za haki, na kuwa katika uaminifu ulinitesa.
76Agano lako aminifu na linifariji, kama ulivyomwahidi mtumishi wako.
77Unihurumie ili niweze kuishi, kwa maana sheria yako ni furaha yangu.
78Wenye kiburi na waaibishwe, maana wamenitukana; bali mimi nitayatafakari maagizo yako.
79Wale wote wanao kucha wewe na wanigeukie, wale wazijuao amri za agano lako.
80Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
81Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
82Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
83Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
84Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
85Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
86Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
87karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.
88Kwa upendo wako thabiti, uniweke hai, ili niweze kuzitii amri zako. LAMEDH.
89Yahwe, neno lako linasimama milele; neno lako limefanywa imara mbinguni.
90Uaminifu wako wadumu kwa ajili ya vizazi vyote; umeiimarisha nchi, nayo inadumu.
91Vitu yote yaliendelea mpaka leo hii, kama vile ulivyosema katika amri zako za haki, maana vitu vyote ni watumishi wako.
92Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningeangamia katika mateso yangu.
93Sitayasahau kamwe maagizo yako, maana kupitia hayo umeniweka hai.
94Mimi ni wako, kwa maana ninayatafuta maagizo yao.
95Waovu hujiandaa kuniangamiza, lakini nitatafuta kuzielewa amri za agano lako.
96Nimeona kuwa kila kitu kina mipaka, lakini amri zako ni pana, zaidi ya mipaka. MEM.
97Oh ni jinsi gani naipenda sheria yako! Ni tafakari yangu mchana kutwa.
98Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.
99Ninauelewa zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa maana ninazitafakari amri za agano lako.
100Ninaelewa kuliko wale wanaonizidi umri; hii ni kwa sababu nimeyashika maagizo yako.
101Nimeiepusha miguu yangu na kila njia ya uovu ili niweze kulitii neno lako.
102Sijaenda kinyume na amri zako za haki, kwa maana wewe umenifundisha.
103Ni jinsi gani maneno yako ni matamu kwenye majaribu yangu, naam, matamu kuliko asali kinywani mwangu!
104Kupitia maagizo yako ninapata utambuzi; kwa hiyo kila njia isiyo ya kweli.
105Neno lako ni taa ya mguu miguu yangu na mwanga wa njia yangu.
106Nimeapa na nimethibitisha, kuwa nitazitii amri za haki yako.
107Nimeteswa sana; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika neno lako.
108Yahwe, tafadhali pokea dhabihu yangu ya hiari ya kinywa changu, na unifundishe amri zako za haki.
109Uhai wangu ziku zote uko mkononi mwangu, lakini bado sisahau sheria yako.
110Waovu wamenitegea mtego, lakini sijapotea mbali na maagizo yako.
111Nimezifanya amri za agano lako kama urithi wangu milele, maana hizo ni furaha ya moyo wangu.
112Moyo wangu umewekwa kuzitii sheria zako milele mpaka mwisho kabisa. SAMEKH.
113Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
114Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
115Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.
116Uniwezeshe kwa neno lako ili niweze kuishi na nisiaibike na matumaini yangu.
117Unisaidie, nami nitakuwa salama; siki zote nitazitafakari sheria zako.
118Wewe huwakataa wale wote wapoteao mbali na sheria zako, maana watu hao ni wadanganyifu na si wakuaminika.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:44-118Zaburi 119:44-118