Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:37-44

Help us?
Click on verse(s) to share them!
37Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
38Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
39Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
40Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
41Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
42ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
43Usiliondoe neno la kweli mdomoni mwangu, maana nimesubiri kwa ajili ya amri zako za haki.
44Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:37-44Zaburi 119:37-44