35Uniongoze katika njia ya amri zako, maana ninafurahi kuenenda katika hizo.
36Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
37Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
38Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
39Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
40Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.