Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:162-175

Help us?
Click on verse(s) to share them!
162Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
170Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
171Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
172Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, maana amri zako zote ni za haki.
173Mkono wako unisaidie, maana nimechagua maagizo yako.
174Ninautamani wokovu wako, Yahwe, na sheria yako ni furaha yangu.
175Naomba niishi na nikusifu wewe, na amri zako za haki zinisaidie.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:162-175Zaburi 119:162-175