Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:159-168

Help us?
Click on verse(s) to share them!
159Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
162Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:159-168Zaburi 119:159-168