Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:152-174

Help us?
Click on verse(s) to share them!
152Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
153Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
154Unitetee na kunikomboa; unihifadhi, kama ulivyo ahidi katika neno lako.
155Wokovu uko mbali na waovu, maana hawazipendi amri zako.
156Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
157Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
158Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
159Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
162Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
163Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
164Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
165Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
166Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
167Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
168Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
169Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
170Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
171Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
172Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, maana amri zako zote ni za haki.
173Mkono wako unisaidie, maana nimechagua maagizo yako.
174Ninautamani wokovu wako, Yahwe, na sheria yako ni furaha yangu.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:152-174Zaburi 119:152-174