Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 119

Zaburi 119:114-161

Help us?
Click on verse(s) to share them!
114Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
115Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.
116Uniwezeshe kwa neno lako ili niweze kuishi na nisiaibike na matumaini yangu.
117Unisaidie, nami nitakuwa salama; siki zote nitazitafakari sheria zako.
118Wewe huwakataa wale wote wapoteao mbali na sheria zako, maana watu hao ni wadanganyifu na si wakuaminika.
119Wewe huwaondoa waovu wa nchi kama takataka; kwa hiyo ninazipenda amri zako thabiti.
120Mwili wangu hutetemeka kwa hofu yako, na ninaziogopa amri za haki yako. AYIN.
121Ninafanya kilicho sahihi na haki; usiniache kwa watesi wangu.
122Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
123Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
124Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
125Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
126Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
127Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
128Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
129Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
130Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
131Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
132Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
133Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
134Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
135Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
136Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
137Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
138Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
139Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
140Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
141Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.
142Hukumu yako ni ya haki milele, na sheria yako ni ya kuaminika.
143Japo dhiki na taabu vimenipata, amri zako bado ni furaha yangu.
144Amri za agano lako ni za haki milele; unipe uelewa ili niweze kuishi. QOPH.
145Nililia kwa moyo wangu wote, “Unijibu, Yahwe, nitazishika sheria zako.
146Ninakuita wewe; uniokoe, nami nitazitii amri za agano lako.”
147NInaamka asubuhi kabla jua halijachomoza na kulia kwa ajili ya msaada.
148Ninatumaini katika maneno yako. Macho yangu yako wazi usiku kucha ili niweze kutafakari juu ya neno lako.
149Sikia sauti yangu katika uaminifu wa agano lako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika amri zako za haki.
150Wale wanaonitesa wananikaribia, lakini wako mbali na sheria yako.
151Wewe uko karibu, Yahwe, na amri zako ni za kuaminika.
152Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
153Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
154Unitetee na kunikomboa; unihifadhi, kama ulivyo ahidi katika neno lako.
155Wokovu uko mbali na waovu, maana hawazipendi amri zako.
156Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
157Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
158Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
159Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
160Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
161Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.

Read Zaburi 119Zaburi 119
Compare Zaburi 119:114-161Zaburi 119:114-161